August 31, 2018


Pazia la michuano ya klabu bingwa Ulaya msimu wa 2018/19 limefunguliwa kwa kupangwa makundi ambapo klabu ya Manchester United inapambana na nyota wake wa zamani Cristiano Ronaldo aliyehamia klabu ya Juventus.

Ronaldo alikipiga na United kwa miaka sita (2003-2009) kisha akachezea Real Madrid kwa miaka tisa na mwezi Julai mwaka huu akahamia klabu ya Juventus, maarufu kama Bibi Kizee wa Turin. Ronaldo ameifunga United mara mbili walipocheza na Real Madrid katika michuano kama hii mwezi Februari na Machi 2013.

United na Juve zimepangwa katika kundi H pamoja na Valencia na Young Boys ya Uswizi.

Bingwa mtetezi Real Madrid wapo katika kundi G pamoja na Roma ya Italia, CSKA Moscow ya Urusi na Plzen ya Ucheki.

Liverpool wapo kwenye kundi gumu la C na watapambana na Paris St. Germain, Napoli na Red Star ya Serbia.

Tottenham pia wapo kwenye kundi gumu lenye timu konge kama Barcelona, PSV na Inter Milan.

Mabingwa wa EPL Manchester City wapo kundi F pamoja na Shakhtar Donetsk, Lyon na Hoffenheim.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic