September 19, 2018

1 COMMENTS:

  1. Wahenga walisema kuvunda halina ubani. Ubani ni manukato au air freshener asilia ya kuondosha au kuziba harufu mbaya ya kitu kichoharibika. Mazaifu ya Mbowe katika utendaji wake wa kazi ya kuiongoza Chadema na kupelekea majanga katika chama hicho lakini leo bila ya aibu wala hisia yakwamba watanzania si wapumbavu, Mbowe anakwenda kukusanya vyombo vya habari na kupotosha uma wa watanzania huku amitumia kauli za matusi akitumia "kisingizio cha hujuma za CCM" kama silaha ya kuziba uozo unaoendelea ndani ya Chadema na kupelekea chama kushindwa kuleta upinzani wa kweli zidi ya CCM. Yafuatayo ni mambo ambayo yanakera na yale ambayo ndio yanayoimaliza Chadema.
    (1) Mbowe na familia yake kuichukulia Chadema kuwa ni taasisi yao binafsi....katika kampeni za uchaguzi mdogo wa ukonga mwanaharakati wa siasa za ukweli kutoka mkoani Moshi alieleza kwa undani kabisa jinsi familia hiyo ya Mbowe ilivyogawana nafasi mabali mbali za kula ndani ya chama hicho tuhuma ambazo watu wengi walitarajia labda Mbowe angekuja juu kwa nguvu zake zote kuzitolea ufafanuzi au kuzikanusha lakini akashindwa kufanya hivyo kwa hiyo tuhuma hizo ni za kweli kabisa.
    (2) Mbowe vs Magufuli? Mbowe ni mwenyekiti wa chama cha Chadema. Magufuli ni mwenyekiti wa CCM. kwa kifupi wasifu wa Magufuli. Ni Msomi wa kiwango cha PhD.Mtaalam mahiri wa kemikia,Na ni mwalimu stadi, Amelitumikia taifa zaidi ya miaka ishirini kwa kujituma na uadilifu mkubwa uliotukuka katika nafasi mabali mbali, Ameishi aiza kwa kujitafutia taaluma ughaibuni na kuzunguka nchi kadhaa za huko na ana mke mmoja na watoto.
    Wasifu wa Mbowe kwa kifupi. Ni mwenyekiti wa Chadema kwa zaidi ya miaka ishirini. Wasifu wa elimu yake haupo wazi lakini inasemekana ni DJ mahiri katika kumbi za Disco wakati huo, uzoefu wa kazi amekuwa mwenyekiti wa Chadema kwa muda mrefu. Ana wake wawili idadi ya watoto haifahamiki.
    Sasa hao ni Makocha wakuu wawili wa kuziongoza timu CCM na Chadema katika kuzipatia ushindi wa timu zao kisiasa na maendeleo na matokeo yeyote yawe ya uchaguzi au kimaeneleo ndani ya vyama vyao hao ndio wapishi wakuu.
    Kuna yanayokera hasa kwa Chadema na kama atatokea mtanzania au taasisi ya kitanzania kutafuta kura ya maoni ili Chadema kifutwe kuwa chama cha siasa basi sitoshangaa hii ni kutokana na upotoshaji unaofanywa na Chadema na viongozi wao pale inapotokea kushindwa uchaguzi. Hakuna ushindi wa CCM utakaokuwa halali mbele ya Chadema lakini ushindi wowote ule wa Chadema zidi ya CCM ni halali na wa haki kabisa? Hii inakera kwani kujenga taifa la watu wenye ustaarabu basi misingi ya kushinda na kushindwa kwa wanaoshindana hasa wanasiasa ni lazima ihishimiwe.
    Ni kweli kabisa kiuhalisia Monduli ni ngome ya CCM na sio ya lowasa au Chadema pale ni nyumbani kwa Sokoine. Chadema kuwahi kupata kiti cha ubunge Monduli ni sawa na mwanamme aliepewa penzi kutoka kwa mwanamke aliemkasirikia mumewe ila ukweli unabakia kuwa mwanamke huyo bado ana mwenyewe.
    Kuhusu malalamiko ya Mbowe kuwa turnout au idadi ndogo ilitojitokeza kupiga kura Ukonga? ni malalamiko ya kipumbavu kabisa kwani kama turnout ni ndogo itakuwa ni kwa wanachama au mashabiki wa Chadema na si wa CCM na hii ni dhahiri inaonesha wananchi wanaoiunga mkono Chadema wamefika mahali wamechoka na chama chao hasa viongozi wao kwa kuwaburuza kama mabumbumbu kutokana na uongozi wa hovyo wa chama chao. Mfano wanachama wakihama Chadema CCM wamewanunua, viongozi wakihama Chadema CCM wamewanunua,madiwani wakihama Chadema CCM wamewanunua? Wabunge wakihama Chadema CCM wamewanunua? No vitu visivyo ingia akilini na ikumbukwe Kila diwani au mbunge au kiongozi wa Chadema hahami bila ya kupima upepo wa watu wake umeekea wapi hivyo Mbowe aache matusi na malalamiko ya kijinga na kupotosha umma wa watanzania kwani hakuna hujuma yeyote ya CCM kwa Chadema bali hujuma ni uongozi mbovu wa chama hicho.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic