September 12, 2018


Na George Mganga

Kaimu Rais wa wa Simba, Salim Abadallah, 'Try Again' amesema klabu hiyo imemaliza tofauti zake na beki wake raia wa Uganda Juuko Murshid.

Kwa mujibu wa Azam TV, Kaimu huyo ameeleza kuwa kwa sasa Murushid yuko huru kuitumikia klabu hiyo, huku mchezaji mwenyewe akiomba ushirikiano kutoka kwa wanachama na mashabiki wa timu hiyo.

Murushid ambaye hajacheza mechi hata moja msimu huu, alikuwa kwao Uganda na juzi aliibukia katika timu ya taifa lake kuitumikia The Cranes dhidi ya Taifa Stars kuwania tiketi ya kufuzu kuelekea AFCON.

Beki huyo anaweza akawa sehemu ya kikosi cha Simba kitakachofanya mazoezi kesho kwenye Uwanja wa Boko Veterani kujiandaa na mchezo wa ligi dhidi ya Ndanda FC.

Simba itakuwa mgeni kucheza na Ndanda Jumamosi ya wiki hii mjini Mtwara kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona.

4 COMMENTS:

  1. Duh kumenoga msimbazi afadhali umerudi baba mwenye nyumba.

    ReplyDelete
  2. Hongera sana kaimu rahisi kwa kulitatua suala la Juuko. Uwepo kwako Simba hakika ni fahari kwa wanasimba wote kwani jitihada zako katika utendaje wako wa kazi kuhakikisha clabu inasonga mbele ni kubwa mno watanzania tunatamani TFF wangekuwa na kiongozi anaelingana na wewe kiutendaji. .

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic