September 10, 2018


Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Juma Mussa ‘Jux’ hivi karibuni ameachia video yake mpya ya Ngoma ya Zaidi ambayo kwa upande wa Tanzania ilikuwa ni namba tano kwenye ngoma zinazotrendi.

Simulizi ya video hiyo ni namna ambavyo Jux alikuwa amezama kwenye penzi zito la mwanadada ambaye alikuwa anasomea sheria na anakwenda mtaani kumtafuta alikomuona kwa mara ya kwanza.

Ukiicheki video hii, Jux ni kama ameweka maisha ya mpenzi wake, Vanessa Mdee ‘Vee Money’ ambaye naye ni mwanasheria wa ngazi ya digrii aliyesomea nchini Kenya kwenye Chuo cha Catholic University of Eastern Africa.

Akizungumzua juu ya hilo, Jux alisema: “Wakati ninaandaa namna video itakavyokuwa sikuwaza kuhusu hilo, lakini baadaye ndiye (Vee Money) alifahamu kwamba kwa namna moja au nyingine video hiyo inaendana na ukweli.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic