September 2, 2018


Straika wa klabu ya Coasta Union ya Tanga, Ali Kiba, jana alishindwa kuwa sehemu ya kikosi cha timu hiyo katika mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya KMC ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo Coastal ilikwenda sare ya bao 1-1 na KMC huku Kiba akiwa jukwaani.

Kiba amesema hajaweza kucheza mechi hiyo kutokana na kutokuwa na mazoezi ikiwa ni baada ya kuwa nje ya nchi ziku za hivi karibuni kwa kazi zake zingine.

Ikumbukwe Kiba ni Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, na hivi karibuni alisafiri kuelekea Canada kwa ajili ya majukumu ya kufanya SHOW.

Baada ya kukosa mechi hiyo, Kiba sasa ataendelea kujifua kwa ajili ya kujiandaa na mechi zingine za ligi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic