NI PIGO? UKIACHANA NA BOCCO, SIMBA KUWAKOSA HAWA WAWILI KUELEKEA MECHI NA YANGA
Na George Mganga
Kuelekea mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga itakayopigwa Septemba 30 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wekundu wa Msimbazi wako kwenye hatihati ya kuwakosa wachezaji wawili.
Mzamiru Yassin na Hassan Dilunga ndiyo wachezaji ambao hawako fiti kiafya mpaka sasa kutokana na kuwa majeruhi, jambo ambalo lilipelekea wasifanye mazoezi jana.
Katika mazoezi ya jana yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Boko Veterani, Yassin na Dilunga hawakuweza kuwa sehemu ya kikosi, na hii ni juu ya afya zao kutokuwa sawa.
Mbali na wawili hao, kuelekea mechi hiyo yenye msisimko wa aina yake, Simba itamkosa pia Nahodha wake, John Bocco ambaye atakuwa anatumikia adhabu ya kuwa na kadi nyekundu.
Bocco alipata kadi hiyo katika mchezo na Mwadui FC uliofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kambarage Shinyanga baada ya kumpiga ngumi mchezaji wa Mwadui wakati pambano likiendelea.
Kikosi cha Mnyama kipana sana
ReplyDeleteKama Mzamiru na Dilunga hawapo fit, wapo Ndemla, Chama, Niyonzima na Mo Ibrahim wote wanacheza hiyo nafasi ya kiungo wa juu
ReplyDeletesimba ina viungo NANE, MASTRAIKA SABA
ReplyDeletehata kama wapo kumi.....hakuna kama dilunga
DeleteMutaelewa tu! Chama hana sub ligi kuu hapa Tz
ReplyDeleteMutaelewa tu! Chama hana sub ligi kuu hapa Tz
ReplyDeleteDaima Mbele,nyuma mwiko
ReplyDelete