September 4, 2018


Uongozi wa klabu ya Yanga umefanikisha kupata vibali vya kazi vya wachezaji wao watatu ambao walikosekana kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Raton Sports.

Wachezaji hao ambao ni Amis Tambwe, Thaban Kamusoko na kipa Klaus Kindoki walikuwa hawana vibali vya kucheza kwenye mashindano hayo yaliyo chini ya CAF.

Tambwe na Kamusoko vibali vyao vilikuwa vimeshamalizika muda wake huku Kindoki alikuwa bado hajapata tangu asajiliwe na mabingwa hao wa kihistoria katika Ligi Kuu Bara.

Baada ya kukamilisha ishu ya vibali hivyo, uongozi Yanga umesema mambo sasa ni shwari na watakuwa wanaoneka kwenye mashindano ya kimataifa wakati ujao.

Aidha, Yanga wameeleza kukipata kibali cha kocha wao mkuu, Mwinyi Zahera ambaye alikaa kwenye mechi dhidi ya Rayon huko Kigali, Rwanda.

1 COMMENTS:

  1. Nilidhani mechi na Rayon Sports ndo ilikuwa ya mwisho kwa Yanga... unamaanisha Yanga wataikoma msimu wa 2019/20?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic