October 21, 2018



Mlinda mlango wa timu ya Yanga ambaye mashabiki wa Simba bado hawajamsahau, Beno Kakolanya amefichua siri ya mafanikio  baada ya kuweza kucheza michezo minne bila kuruhusu bao katika mechi dhidi ya Simba,Singida United,Mbao FC na Alliance.

Kakolanya amesema  kikubwa  kinachomsaidia kuwa katika ubora  ni kujiamini  katika kazi yake anayoifanya pamoja na maelewano mazuri ya safu ya ulinzi.

"Jambo la kumshukuru Mungu kwa kuweza kufikia mafanikio haya,lengo langu ni kuweza kuendeleza rekodi hii katika michezo mingine inayofuata.

"Maelewano yaliyopo kwa safu ya ulinzi yanasaidia kuwa katika ubora ambao nipo nao, ninazidisha umakini kila ninapokuwa uwanjani ili kufanikiwa "alisema .

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic