KISA SULUHU DHIDI YA YANGA, MKUU WA MKOA MTWARA AIBUA MAKUCHA
Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa, amesikitishwa na matokeo ambayo Simba iliyapata dhidi ya Yanga kwa kumaliza mchezo bila kufungana.
Byakanwa ameeleza kuwa imemsikitisha yeye kama mnazi wa Simba kwa kwenda suluhu na Yanga ambayo ilikuwa dhaifu kuliko wao.
Kiongozi huyo amesema uwepo wa mashuti mengi ya kufunga kwao na umiliki wa mpira hauna yoyote na badala yake furaha pekee ilipaswa waibuke na ushindi.
Byakanwa amefunguka akiamini kuwa kikosi cha Simba ni kipana hivyo kwenda suluhu ya Yanga ni jambo ambalo limeshangaza na hakutegemea.
"Sijafurahishwa na matokeo dhidi ya Yanga kwa maana ya kwamba ni timu ambayo tunaizidi kwa ubora msimu huu, sikutegemea kabisa lakini ndiyo mpira ulivyo, tulistahili kushinda" alisema.
Ndiyo,ni ngumu kuelewa Kwa sabsbu Yanga waliwazidi simba kimbinu na ujanja,waksti simba imecheza Moira wa mazoea kufurajisha jukwaa.Moira Wa photovoppy Kama alivyo ainisha Zshera.inantakiwa .mbinu na ujanja zaifi ikiwa tunataka matokeo.
ReplyDelete