October 13, 2018


Na George Mganga

Uongozi wa klabu ya Mtibwa Sugar umeendelea kuzililia fedha zake za ubingwa wa Kombe la Shirikisho 'Azam Sports Federation CUP' ilizozipata kwa kutwaa taji hilo.

Mpaka sasa bado Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) halijakabidhi fedha hizo kwa Mtibwa ambao walibeba ubingwa ka kuifunga Singida United mechi ya fainali kwa mabao 3-2.

Kwa mujibu wa Msemaji wa klabu hiyo, Thobias Kifaru, amesema wao kama klabu wanasikitishwa kutokupokea fedha hizo hadi leo.

Kifaru ameeleza kushangazwa na TFF huku akinena hawezi kuzungumza mengi kwa sababu anaweza akaonekana kama tatizo kwa shirikisho hilo.

"Hauwezi amini mpaka sasa bado hatujapokea fedha hizo, nakosa mengi ya kuzungumza na inashangaza kwakweli" alisema.

Mtibwa ilifanikiwa kuwa bingwa baada ya kuilaza Singida mabao hayo matatu kwa mawili, mchezo uliopigwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Juni 2 2018.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic