Uongozi wa timu ya Azam FC, umejitangazia ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambao unashikiliwa na Simba FC, kutokana na kuwa nafasi ya kwanza na kucheza michezo 12 bila kupoteza wakiwa na pointi 30.
Ofisa habari wa Azam FC, Jaffari Maganga amesema kuwa hakuna ubishi kwa sasa kikosi bora ni Azam na endapo kutatokea na janga kwenye taifa wataiwakilisha nchi.
"Kwa sasa ipo wazi sisi ndio mabingwa maana kama bahati mbaya kutatokea na majanga ya asili, basi bingwa ni Azam FC, nasi tutawaakilisha nchi kwenye michuano mikubwa tunapaswa tuheshimiwe," alisema.
Kesho Azam FC watacheza na Ruvu Shooting katika uwanja wa Chamazi majira ya saa moja usiku ikiwa ni mwendelezo wa Ligi kuu.
Ofisa habari wa Azam FC, Jaffari Maganga amesema kuwa hakuna ubishi kwa sasa kikosi bora ni Azam na endapo kutatokea na janga kwenye taifa wataiwakilisha nchi.
"Kwa sasa ipo wazi sisi ndio mabingwa maana kama bahati mbaya kutatokea na majanga ya asili, basi bingwa ni Azam FC, nasi tutawaakilisha nchi kwenye michuano mikubwa tunapaswa tuheshimiwe," alisema.
Kesho Azam FC watacheza na Ruvu Shooting katika uwanja wa Chamazi majira ya saa moja usiku ikiwa ni mwendelezo wa Ligi kuu.
duh mechi 12 mmeanza mbwembwe
ReplyDeleteDu ligi kumbe imeisha
ReplyDeleteHata raundi ya kwanza haijaisha mnaanza tambo! Kwani mmeshacheza na Mnyama? Kuna mechi nyingi za away pia mtapoteza, Ni mapema mno kuanza tambo.
ReplyDeleteHa ha ha ha ha subiri tutaona.
ReplyDeleteHata mzunguko wa kwanza bado umeanza tambo pole sana ila jitahidi kila jambo linawezekana.
ReplyDeleteNafikiri msemaji hana jipya kwake ameona mechi 12 ni za kutangazia ubingwa wa Ligi Kuu Bara.
ReplyDeleteOmary Kausimbe,
ReplyDeleteHayo ni maneno ya mkosaji huyo msemaji wa azam naona hana cha kuongea teh teh
Unaomba kuheshimiwa kwa kuongoza ligi baada ya michezo 12 unashindwa kutoa heshima kwa bingwa mtetezi mana kombe halitolewi pakitokea majanga kama unavyoomba wewe yatokeee
ReplyDeleteCheche hajui kuwa leo Alhamisi pia atakuwa na kazi nzito usiku?
ReplyDelete