Zana Coulibaly beki wa kulia raia wa Burkinafaso leo amekamilisha dili la kusajiliwa na Mabingwa wa nchi Simba SC. Pichani akisaini mkataba wa miaka miwili mbele ya Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Simba, Crescentius Magori.
Coulibaly aliwahi kung'ara na Asec Mimosa, amejiunga na Simba kuongeza nguvu upande wa kulia kutokana na Shomari Kapombe kuwa majeruhi.
Kapombe aliumia akiwa katika kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars kilichokuwa kinajiandaa kucheza na Asec Mimosa.
This is simbaaaaa bhana bado yule mshambuliaji hatari wa Ghana, fanyeni mambo chap hawa jamaa wanaongea sanaaaaa.
ReplyDeleteSaaaafiiii
ReplyDelete