November 19, 2018


Uongozi wa Mwadui FC, umesema kuwa wataisimamisha timu ya Yanga katika uwanja wa Kambarage ili kuweza kuvunja rekodi ambayo haijavunjwa mpaka sasa katika michezo 10 waliyocheza timu ya Yanga.

Katika michezo 10 ambayo Yanga wamecheza hawajapoteza hata mmoja zaidi ya kutoa sare michezo 2 na kushinda michezo 8 na wamejikusanyia pointi 26 wakiwa nafasi ya 3 kwenye msimamo.


Katibu wa Mwadui FC, Ramadhani Kilao amesema wanatambua ubora wa wapinzani wao ila hawana hofu kwa kuwa hesabu zao ni kuchukua pointi tatu.


"Hatutishwi na ubora wa kikosi cha wapinzani wetu, nasi pia tuna uwezo wa kuwasimamisha katika uwanja wetu wa Kambarage kwa kuwa wanaujua vizuri hivyo tumejipanga kuchukua pointi tatu nyumbani," alisema. 


Mchezo wa Yanga na Mwadui utachezwa Novemba 22 katika uwanja wa Kambarage utakuwa ni wa kwanza kwa Yanga kucheza mkoani.

1 COMMENTS:

  1. Kuna mtandao umesukwa kutokea Serikalini, Wizarani, Magazeti, waandishi wa Habari, BMT na TFF, Body ya Ligi na baadhi ya wanachama maarufu wa Yanga, kwa lengo la KUIHUJUMU NA KUIDHOOFISHA YANGA....mfano Uchaguzi angalia mchakato mzima....kabla, na wakati wa uchaguzi wenyewe. Angalia kwenye mechi ya kirafiki Namungo njoo kwenye wachezaji wa Timu za Taifa (u23 na Taifa Stars) hawajaripoti kambi ya Yanga kwenda kucheza mechi na mwadui...Bodi ya Ligi ingesogeza mechi yao ili kuruhusu wachezaji wao wajiunge na timu hawakufanya hivyo....ila Simba wameruhusiwa. Ukija kwenye mchakato wa ratiba za mechi zilizopangwa na bodi ya ligi....njoo uangalie sarakasi za uchaguzi...Swali Kwanini kakolanya, Yondani, ninja, kabwili na Paulo Godfrey hawatajiunga na Timu ili kuwahi mechi na Mwadui. Wenye akili tushajua hili...

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic