November 21, 2018


Beki wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Erasto Nyoni, amewaambia Watanzania kuwa, bado hawajamaliza kazi, hivyo waendelee kuwasapoti.

Nyoni ametoa kauli hiyo baada ya wikiendi iliyopita timu hiyo kukubali kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Lesotho ukiwa ni mchezo wa kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa Afrika (Afcon).

Katika mchezo huo wa Kundi L uliochezwa kwenye Uwanja wa Setsoto uliopo Maseru, Lesotho, Taifa Stars ilitakiwa ishinde ili ifuzu moja kwa moja, lakini haikuwa hivyo.

Nyoni ambaye kwenye mchezo huo alikuwa nahodha, alisema: “Watu wasichukulie kama vile ndiyo kazi imeisha, hapana, bado tuna nafasi ya kufanya vizuri na kufuzu Afcon.

“Tunawaomba Watanzania waendelee kutuunga mkono, tunajua matokeo haya hayakuwa mazuri, lakini tunawataka watupe sapoti tuweze kufanya vizuri dhidi ya Uganda.”

Ikumbukwe kuwa, Taifa Stars ambayo kwa sasa inashika nafasi ya tatu kwenye kundi hilo ikiwa na pointi tano sawa na Lesotho, inatakiwa kushinda mechi ya mwisho dhidi ya Uganda, huku ikiomba Lesotho ipoteze mbele ya Cape Verde au kutoka sare ili ifuzu Afcon.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic