Ofisa habari wa Singida United, Cales Katemana amesema uongozi wa Simba umeamua kuwawekea ugumu kwa washambuliaji wao waliotaka kuwasajili kutokana na masharti yao.
Singida United wana mpango wa kusajili kwa mkopo wachezaji wawili kutoka Simba ambapo waliandika barua ili waweze kupata huduma ya wachezaji hao ila mpaka sasa bado mambo yamekuwa magumu.
"Uongozi wa Simba bado hatujafika nao muafaka mzuri kwa wachezaji wao ambao tulikuwa tunahitaji kuwachukua kwa mkopo, kama mipango itazidi kuwa migumu kwao
tutatafuta wachezaji wengine," alisema.
Singida United tayari wamenasa saini ya mshambuliaji mwenye uraia pacha wa Norway na Liberia Dauda Bortu kwa mkataba wa miaka miwili wana mpango wa kupata washambuliaji wawili kutoka Simba.








0 COMMENTS:
Post a Comment