MBELGIJI SIMBA AANIKA MBINU HIZI KIBOKO KWA MBABANE
Wakati leo Jumanne Simba ikiwa ugenini kucheza na Mbabane Swallows ya Eswatini, Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems, ameweka wazi kwamba plani yake ni kuimaliza mechi hiyo mapema kwa kupata bao la dakika za nwanzoni ambalo litawachanganya wapinzani wao.
Simba watakuwa nchini Eswatini kwa ajili ya mechi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya ule mchezo wa awali jijini Dar es Salaam kushinda 4-1.
Mbelgiji huyo amesema kwamba licha ya kuelewa ugumu ambao upo katika mechi hiyo, hasa wakiwa ugenini, wamejipanga, ambapo plani yao ni kupata bao hilo la mapema ambalo litachangia kwao kucheza kiutulivu.
“Tunajua kwamba tupo ugenini na haiwezi kuwa mechi nyepesi hata kidogo kwani wenzetu nao watataka kuonyesha kwamba wapo nyumbani ambapo ni muhimu kuibuka na ushindi kwa upande wao.
“Kitu kikubwa ambacho tumepanga kukifanya ni kucheza kwa utulivu na kutambua kwamba tulipata mabao mengi kule nyumbani, hivyo ni lazima tulinde ushindi wetu. Kitu kikubwa tutakachofanya ni kutoruhusu bao kwetu lakini pia tutajitahidi tufunge bao la mapema ambalo litakuwa msaada mkubwa kwetu,” alisema Mbelgiji huyo.
CHANZO: CHAMPIONI
0 COMMENTS:
Post a Comment