December 4, 2018


Kamati ya Usa­jili ya Yanga, rasmi imethibitisha kufikia uwezekano wa asil­imia 90 kuwasajili wachezaji watatu katika usajili huu wa dirisha dogo.

Hiyo, ikiwa ni siku chache tangu Yanga imshushe winga wake raia wa DR Congo, Re­uben Bomba ambaye yupo nchini kwa ajili ya kufanya mazungumzo kabla ya kum­sainisha mkataba wa kukipiga Jangwani.

Timu hiyo, tofauti na kuwa na mazungumzo na Mkongo huyo, zipo tetesi za kumsajili beki wa Lipuli FC, Ally Mtoni ‘Sonso’ na mshambuliaji wa Mbeya City, Eliud Ambokile ambaye ni kinara wa mabao katika Ligi Kuu Bara.

Kwa mujibu wa Champi­oni, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Hussein Nyika, alisema kwa asilimia 90 mipango yao ya usajili imekamilika, hivyo wakati wowote watawasajili wachezaji hao.

“Niwatoe hofu mashabiki wa Yanga kwa kuwaambia kuwa mipango yetu ya usa­jili imekamilika kwa asilimia 90, hivyo kilichobakia ni ku­malizana na wachezaji hao aliowahitaji kocha.

“Tayari kocha ameshatu­kabidhi ripoti yake ya usa­jili akihitaji winga, beki wa kati, mshambuliaji na kiungo mmoja mkabaji ambao tayari tumewapata, kilichobakia ni kuwasajili pekee.

“Hakuna kitaka­choshindikana kwetu, licha ya uchumi wetu kuyumba, matarajio yetu ni kuona timu ikifanya vizuri ka­tika mzunguko wa kwanza baada ya kukamilisha ma­hitaji ya kocha katika usajili wetu,” alisema Nyika.

3 COMMENTS:

  1. Safi sana yanga,timu ya taifa hii haiwezi kuyumba alafu eti nchi isiyumbe lazima muingalie kama mnavyoiangalia CCM tena kwa jicho la tatu.

    ReplyDelete
  2. mmelipa madeni ya usajili ya wachezaji wenu

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic