February 28, 2019


Wakati kikosi cha Simba kikiendelea kula viporo vyake, uongozi wa timu hiyo umesema malengo yake ni kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwa misimu 10 ijayo mfululizo.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara, ameeleza kwa kikosi walichonacho hivi sasa kinawapa jeuri hiyo.

Manara ameeleza kuwa wanataka kuifikia na ikiwezekana kuizidi mataji Yanga ambayo imetwaa mara 27 huku Simba wakiwa wamechukua mara 18 tu.

Simba wikiendi hii itakuwa na kibarua kingine cha ligi mjini Shinyanga na kuelekea mechi hiyo Manara amesema wamejipanga vizuri.

Tayari kikosi kipo njiani na Kocha Mkuu, Mbelgiji Patrick Aussems amesema wanaenda kupigania alama tatu muhimu kujiwekea mazingira mazuri ya kuchukua ubingwa.

5 COMMENTS:

  1. Inatakiwa transparent and accountability katika bodi ya usajili uzingatiwe,kama club imeamua kusajili mchezaji basi ni bora vigezo na sifa viwekwe wazi kabla yakufanya usajili,me naona hilo linaweza likasaidia timu kufanya vizuri,mchezaji aanikwe wazi kuanzia alikoanzia kucheza soka mafanikio yake binafsi katika kuchukua mataji,mafanikio ya kitimu katka kuisaidia kupata matokeo bora,na je ana uwezo gani kwa sasa pia thamani kulingana na uwezo wake,kama tumedhamiria jamani bora ifanyike haswa kwasababu inawezekana tena kwa kiwango cha juu kabisa,na hii sio kwa simba tu hata azam,yanga na clubs zingine za kibongo inawezekana, shime jamani.

    ReplyDelete
  2. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
  3. Hukutaja inakwenda kupambana na yimu gani

    ReplyDelete
    Replies
    1. Aya ya pili kutoka chini......."Simba wikiendi hii itakuwa na kibarua kingine cha ligi mjini Shinyanga na kuelekea mechi hiyo Manara amesema wamejipanga vizuri".

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic