KIONGOZI YANGA: TFF WALIUMIZWA NA MATOKEO KAGERA WAKAPANGA MATOKEO MECHI NA KMC
Wakati kikosi cha Simba kikishuka dimbani Uwanja wa Karume leo kumenyana na Biashara kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara, Mjumbe wa Baraza la Wazee Yanga, Ibrahim Akilimali, amesema kuwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) liliumizwa na matokeo ya timu hiyo mkoani Kagera.
Akilimali amesema kuwa baada ya Simba kufungwa na Kagera mabao 2-1 na kuamua kupanga matokeo ya mchezo uliofuata na KMC FC uliopigwa Uwanja wa CCM Kirumba.
Mzee huyo ameeleza TFF iliyo chini ya Rais Wallace Karia haikuwa na wakati mzuri baada ya kupoteza mbele ya Kagera na ili mipango isiharibike waliamua kupanga mechi dhidi ya KMC kuipa urahisi wa kushinda.
Katika mechi dhidi ya KMC Simba walifanikiwa kushinda kwa mabao 2-1 huku penati ya ushindi kwa Simba ikileta gumzo kubwa kwa namna ilivyopatikana.
Akilimali alieleza kuwa penati hiyo ilikuwa ya mipango na badala yake akasema mchezo huo haukuwa na maana yeyote kwani tayari ulikuwa una matokeo kabla ya kuchezwa.
HAMNA KITU. HUYU SI NDIO MZEE ALIYEMKATAA MANJI KUWA MWENYEKITI HALAFU KARUDI KUMLAMBA MIGUU KWAAJILI YA KUPEWA BAHASHA ?
ReplyDeleteKwani si mmebebwa lakini,najua ukweli unauma vumilieni
DeleteNYIE MAFALA WA YANGA MUMESHINDWA KUCHEZA MECHI ZENU NA KUSHINDA MUNATEGEMEA KINA kmc WASHINDE ILI MUBEBE UBINGWA PUMBAVU ZENU WOTE PAMBANENI NA HALI ZENU KILA MTU ACHEZE MECHI ZAKE
DeleteDOGO BADO UNAHITAJI KUJIFUNZA KISWAHILI ILI UWEZE KUANDIKA KISWAHILI FASAHA
DeletePia nakumbuka wanna yanga walimkataa Keanu ni yeye aliemtilia guu Manji leo hii yanga isingukuwa katika shida ya kipato. Nafukuru Kwanza hukutana na Zahera na baadae kutoa msimamo wako. Hapo nyuma mara nyingi wapo waliokuwa wakitamka kumwambia Manji "ondoka utuwachie yanga yetu" na akasikia huo wito na akaondoka
ReplyDeleteSimba alicheza na Alliance baada ya mechi nä Kagera .Huyu mzee ameezeka kubaya.Lakini ndio msemaji maarufu wa mapoyoyo.
ReplyDeleteHaka Kazee Kana Shida, Nataka Nimkumbushe Yanga Vs Simba 1-1 Wafungaji Akiwa Tambwe Na Kichuya, Goal La Ajibu Lilikataliwa Likakubaliwa Gol La Mkono La Tambwe Mkude Akatolewa Kwa Red Card Waamzi Wakafungiwa Lakini Je, Matakoe Yalibadilishwa Iwe 1-0 Jibu Ni Hakuna Sasa Et Kanataka Simba Ipate Sale Na KMC Swali Simba Vs Ailliance Matokeo Haya Kupangwa?
ReplyDeletempira mbinu Akilimali waache wenye pesa wacheze unashangaa mkubwa kuzama?
ReplyDeleteNa badoo,, ,kuna penati kama 8 hv bado zipo kwenye fridge
ReplyDeleteMawazo mufilisi.Nilianza kuwaonea huruma pale waliposhangilia kufungwa goli moja na Simba.
ReplyDelete