Juma amesema kuwa walijipanga kupata matokeo mbele ya Simba ila walishindwa kutokana na kushindwa kutumia nafasi ambazo walizipata.
"Tumepoteza kwa kuwa tulishindwa kutumia nafasi ambazo tumezipata, ila bado tuna nafasi ya kubaki kwenye ligi kwa kuwa mchezo mmoja mkononi tunao na tunahitaji pointi moja.
"Mchezo wetu unaofuata tutakuwa Tanga hivyo tutapambana kupata pointi moja ili tubaki kwenye ligi msimu ujao," amesema Juma.
Singida United imecheza michezo 37 imejikusanyia jumla ya pointi 45 ikiwa nafasi ya tisa kwenye msimamo, mchezo wake wa mwisho itacheza na Coastal Union Tanga.
Naona bado baadhi ya watanzania hawajaridhika na uhalali wa ubingwa aliouchukua Simba...sijui shida iko wapi? maana mimi bado sijaiona!
ReplyDelete