May 2, 2019



FT: Yanga 1-2 Prisons

Uwanja : Uhuru


Wafungaji: Papy Tshishimbi dk ya 23 kwa Yanga, Heritier Makambo dk ya 66.
Ismail Kada dk ya 33 kwa upande wa Prisons

MCHEZO wa leo uliochezwa Uwanja wa Uhuru kati ya Yanga ya Dar dhidi ya Tanzania Prisons ya Mbeya umekamilika kwa Yanga kuibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 2-1.

Yanga walianza kupata  kwa bao la kuongoza lililofungwa na Pappy Tshishimbi dakika ya 23 kwa kichwa akiunganisha pasi ya Ibrahim Ajibu.

Tanzania Prisons walipata bao la kusawazisha kupitia kwa Ismail Kada kupitia kona iliyopigwa na Salum Kimenya dakika ya 33.

Makambo alifunga bao la pili kwa Yanga akimalizia pasi ya Paul Godfery dk ya 66.



8 COMMENTS:

  1. Kulingana Na Uchambuzi Wa Wachambuzi Wa Azamtv Abdalla Shaibu Ili Faa Apewe Kadi Nyekundu Lakin Kutokana Na Marefalii Kumuogopa Zahera Na Kelele Zake Ameaamua Atumie Busara Kwa Kutoa Kad Ya Njano

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kwani Azam Tv ni waamuzi wa mchezo wa Soka? Zahera ni nani mpaka awe juu ya sheria 17 za soka?

      Delete
    2. Tuache ushabiki...pale yule mchezaji angepewa red card...tungesikia ni hujuma ya kuipa timu fulani ubingwa..

      Delete
  2. Kwani nyie mnapopiga kelele na kulalama ni waamuzi wa soka?Au ikiwa kwenu basi refa mwamuzi wa mwisho ikiwa kwa Simba sheria zinavunjwa?Udhaifu ni ugonjwa .

    ReplyDelete
  3. Hivi hawa waandishi wa hiki kiblog wanajitambua kweli? kichwa cha habari kuhusiana na matokeo ni tofauti na matokeo ya uwanjani.Kaaazi kweli kweli!!!!!

    ReplyDelete
  4. Kichwa cha habari kinaonyesha Yanga 1 Prisons 2,daaah! Waandishi kaaazi ipo!

    ReplyDelete
  5. Hawa waandishi wetu mtihani kweli kweli, sijui huwa wanawahi mwapi wanashindwa hata kuptitia na kuhariri habar zao.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic