July 16, 2019



KOCHA Mkuu wa Biashara United, Amri Said amesema kuwa timu yake itaweka kambi Tarime kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao unaotarajiwa kuanza Agosti 23, Julai 20.

Akizungumza na Saleh Jembe, Said amesema kuwa kwa sasa kinachowachelewesha kuanza kambi ni ukata hivyo mambo yakikaa sawa wataingia kambini.

“Kwa sasa bado hatujaanza kambi, ilibidi tuanze Julai 15 mambo hayajawa sawa kutokana na tatizo la uchumi, ila mpaka Julai 20 mambo yatakuwa sawa na lazima tuanze kujiaanda kwa ajili ya msimu ujao kwani ratiba imebana.

“Timu itaweka kambi Tarime na tumepanga kucheza mechi nyingi za kirafiki ili kuandaa kikosi makini, nina mani tutafanya vizuri msimu ujao wadau na mashabiki waendelee kutupa sapoti,” amesema Said.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic