July 1, 2019




KOCHA Mkuu wa KMC, Jackson Mayanja amesema kuwa kwa sasa ameshaanza kazi kukinoa kikosi hicho kwa ajili ya michuano ya Kagame Cup inayotarajiwa kuanza mwezi Julai nchini Rwanda.

KMC imepangwa kundi A ambalo lina timu kama TP Mazembe ya Congo, Rayon Sports ya Rwanda na Atlabara ya Sudan Kusini na bingwa mtetezi ni Azam FC.

Mayanja amesema atawatumia wachezaji wote waliosajiliwa na KMC bila kuwabagua kwani anaamini wana uwezo mkubwa hali inayompa nguvu ya kuleta ushindani.

Mpaka sasa tayari KMC  imesajili majembe mapya Saba huku  nyota 14 wakiongeza kandarasi kuitumikia timu hiyo ambayo itashiriki pia michuano ya kimataifa kwenye kombe la Shirikisho.

Majembe mapya ni:-Salim Aiyee ambaye amesaini kandarasi ya miaka miwili akitokea Mwadui FC, Mohamed Samata amesaini kandarasi ya miaka mitatu akitokea Mbeya City, Ismail Gambo amesaini miaka mitatu ametokea Azam FC.

Vitalis Mayanga amesaini kandarasi ya mwaka mmoja ametokea Ndanda FC, Kenny Ally amesaini kandarasi ya miaka miwili ametokea Singida United na  Amos Charles amesaini miaka mitatu ametokea Mbao FC na Ramadhan Kapera amesaini kandarasi ya miaka miwili akitokea Kagera Sugar.

Walioongeza mikataba ni James Msuva (2), Aron Lulambo, Juma Kaseja, Denis Richard, Rayman Mgungila, Ally Ramadhan, Kelvin Kijiri, Hassan Kabunda, Charlse Ilanfia, Cliff Buyoya, Sadala Lipangile, Rehan Kibingu, Omary Ramadhan, Abdul Hillary wote wameongeza kandarasi ya miaka mitatu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic