July 3, 2019





KASSIM Khamis, mshambuliaji wa Kagera Sugar ambaye alifunga moja ya bao walipocheza na Simba uwanja wa Kaitaba ambapo Simba ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-1 yupo kwenye mazungumzo ya mwisho na Azam FC.

Habari za ndani zimeeleza kwamba kwa sasa Azam FC tayari wamekamilisha usajili wa wachezaji wa nje hivyo anahitajika mchezaji mmoja wa ndani ambaye ataongeza nguvu ndani ya kikosi.

“Tayari wachezaji wa nje kocha Ettiene Ndayiragije ameshamalizana nao hivyo kwa sasa anamtafuta mchezaji mmoja wa ndani ambaye ataleta ushindani, yule mshambuliaji wa Kagera Sugar,  Kassim anaangaliwa kwa ukaribu,” kilieleza chanzo.

Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffari Mganga amesema kuwa suala la mchezaji atakayesajiliwa ndani ya Azam FC lipo mikononi mwa kocha mwenyewe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic