July 2, 2019


Kazi ya kusajili wakali watakaohakikisha kikosi cha Mabingwa kinazidi kuwa tishio kwa wapinzani inaendelea.

Mshambuliaji raia wa Congo DR, Deo Kanda (29) amejiunga na Mabingwa wa nchi Simba SC. 

Kanda amesaini mkataba wa mwaka mmoja kukipiga Msimbazi akitokea TP Mazembe ambapo alikuwa mmoja wa wachezaji ambao waliiwezesha kushinda Ubingwa wa Afrika mwaka 2009, 2010 (aliifungia goli kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Esperance) na 2013.

Kanda pia akiwa ameshiriki Kombe la Dunia la Vilabu mwaka 2009, 2010, 2013.

5 COMMENTS:

  1. Mbona hayupo Timu ya Taifa ya DRC? Tuliahidiwa kila pro atakayesaini Simba mwaka huu awe ana namba kwenye National team.

    ReplyDelete
  2. Mchezaji kacheza kombe la Dunia kwa ngazi ya klabu halafu mtu anauliza mbona timu ya taifa hayumo? Huyu keshapita ngazi ya taifa ni wa ngazi ya Dunia

    ReplyDelete
  3. Nimekumbuka wakati Clatous Chama anasajiliwa Simba na kutambulishwa pale Simba day hakupokelewa kwa vishindo lkn sasa hivi ni mmoja wa wachezaji anayeimbwa kila siku pale Msimbazi.Ligi za kitaifa na kimataifa zote ni mwezi ujao August na ndio tutawahukumu.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic