July 2, 2019



Na Saleh Ally, Cairo
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Emmanuel Amunike ameendelea kusisitiza kwamba yeye hana cha kulaumiwa.

Amunike amesema mara baada ya Stars kupoteza mchezo wake wa mwisho katika michuano Afcon.

Taifa Stars ilifungwa mechi zote tatu za michuano hiyo kwa kukubali mabao nane katika mechi tatu huku ikifunga mawili.

Baada ya mechi ya mwisho baada ya Stars kulala kwa mabao 3-0 kutoka kwa Algeria, Amunike amuse a hana cha kulaumiwa.

“Nilaumiwe kwa lipi? Mimi ni kocha na timu uliiona. Hapo ndipo tulipofikia na nilichofanya sikuwa na zaidi ya kuongeza,” alisema.

Hata alipoulizwa kwamba ana maanisha hakuwa na uwezo wa kuongeza chochote cha kuiokoa au ana maanisha hakuwa na uwezo zaidi ya hapo, akajibu.

“Mimi nimemaliza, indigo tulipofikia, ahsante.”

MECHI ILIZOPOTEZA TAIFA STARS:
Vs Senegal 2-0
Vs Kenya 3-2
Vs Algeria 3-0


5 COMMENTS:

  1. Sasa kaonesha dharau gani huo ndio ukweli wenyewe tatizo tunapenda maneno ya kuriwazana tuu. Timu imeweka kambi wiki moja Dar ikamalizia Misri wenzenu wameweka kambi za maana kujiandaa eti mnategemea mpate ushindi kirahisi hovyo kabisa. Tuwekeze siriasi kwenye mpira tuache porojo.

    ReplyDelete
  2. HIVI ULITAKA KOCHA ASEME NINI ZAIDI? NI JUU YA MWAJIRI WAKE SASA KUAMUA KAMA ANAONA UWEZO WA KOCHA UMEFIKIA KIKOMO NA KAMA ANATAKA MAFANIKIO ZAIDI AU YA HAPO TULIPOFIKA YAMETOSHA.

    ReplyDelete
  3. Tatizo waandishi wetu hata lugha shida huenda hakumuelewa kabisa kocha na kibaya zaidi wamezoea interview simple kutoka kwa kina Julio na Masau Bwire. Jiongezeni wakubwa.
    Hapo kilichobaki ilikuwa aingie mwenyewe kocha

    ReplyDelete
  4. Kocha bomu zamani sana ila TFF ni bomu zaidi.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic