UONGOZI wa
Alliance FC 0 kuwa msimu ujao utawafundisha soka la darasani vigogo wa
ligi ikiwa ni pamoja na Yanga, Simba pamoja na Azam FC.
Alliance
ambayo msimu ujao utakuwa ni msimu wake wa pili kwa sasa ipo chini ya Kocha
Mkuu, Athuman Bilal aliyekuwa akiinoa Stand United na amesaini kandarasi ya
miaka miwili.
Akizungumza
na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Alliance, Jackson Mwafulango amesema kuwa
msimu mpya watakuwa tofauti zaidi ya msimu uliopita.
“Msimu
uliopita tulikuwa na sera ya kusambaza misumari ya upendo, safari hii
tumejipanga kabisa kuwapa mpira wa darasani wapinzani wetu na kupata matokeo
chanya.
“Unajua
msimu uliopita haimaanishi kwamba kupoteza mbele ya Simba na Yanga
hatukuwapeleka darasani hapana walituzidi uzoefu ila kwa sasa tumejipanga
kuwarudisha darasani na matokeo tunachukua,” amesema Mwafulango.







Brother Mwafulango angalia maneno yako yatokuponza kama Masawe Bwire.Kila la kheyr
ReplyDelete