September 28, 2019




UONGOZI wa Azam FC umesema kuwa kwa sasa hauna cha kuhofia mbele ya wapinzani wao Triangel United kwa kuwa wamejifunza kupitia makosa na leo watapindua meza kibabe.

Azam FC ilikubali kuchapwa bao 1-0 kwenye mchezo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho uliochezwa uwanja wa Azam Complex hivyo leo wana kibarua cha kufunga mabao zaidi ya mawili.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Azam Fc Jaffary Maganga amesema kuwa mipango ipo kamili na wana sapoti kubwa ya mashabiki wa Zimbabwe.

“Tupo vizuri na tuna amini tutapata matokeo chanya kwenye mchezo wetu wa pili ukizingatia kwamba kuna mashabiki wa Azam FC ambao wapo huku Zimbabwe wameahidi kutupa sapoti.

“Mipango ya Kocha ipo sawa ni suala la muda tu kupindua meza, mashabiki waendelee kutuombea dua ili tufanye vema na turejee na ushindi Bongo,” amesema Maganga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic