ZDRAVCO Logarusic,
aliyekuwa Kocha wa Simba zamani kwa sasa anaifundisha timu ya Taifa ya
Sudan amesema kuwa Azam FC na Yanga zina deni kubwa kwa Taifa la Tanzania
ambalo uwezo wa kulilipa lipo miguuni mwa wachezaji endapo wataacha papara
wakiwa kwenye lango.
Azam na Yanga, leo zinashuka
uwanjani ambapo Yanga inapeperusha bendera kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika na
itamenyana na Zesco United huku Azam FC ikiwakilisha Taifa kwenye Kombe la
Shirikisho Afrika itamenyana na Triangel United.
Akizungumza na Saleh Jembe, Logarusic amesema kuwa aliutazama mchezo wa kwanza wa Yanga
dhidi ya Zesco na kuona namna ilivyolazimisha sare ya kufungana bao 1-1 huku
Azam FC ikipoteza mbele ya Triangle United ya Zimbabwe kwa kufungwa bao 1-0.
"Nimeona namna
Yanga inavyocheza pamoja na wapinzani wao walivyo si timu ya kubeza Zesco ipo fiti,
hata Azam pia bado wapinzani wao ni wagumu ila wanafungika iwapo wachezaji hasa
safu ya ushambuliaji Ikipunguza papara.
"Tanzania kuna
vipaji na wachezaji wengi wanajisahau wakiwa uwanjani, kwa upande wa wakilishi
wa Tanzania Yanga na Azam wana kazi kurejesha furaha na kufunga mabao mengi ya mapema
inawezekana wakiamua," amesema.
Timu mbili ili kusonga
hatua inayofuata ni lazima zishinde, ikitokea zikakwama Azam itakuwa
imefungashiwa virago jumla huku Yanga akidondokea kwenye Kombe la Shirikisho.







0 COMMENTS:
Post a Comment