September 30, 2019



AZAM FC mabingwa watetezi wa Kombe la FA, wamekubali yaishe kwenye michuano ya Kimataifa baada ya kutolewa na Triangel United kwenye Kombe la Shirikisho hatua ya awali.

Azam FC iliyo chini ya Kocha Mkuu, Ettiene Ndayiragije  imefungashiwa virago baada ya kufungwa jumla ya mabao 2-0 na wapinzani wao Triangle United ambao waliifunga nje ndani.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffary Maganga amesema kuwa hesabu zao ilikuwa kupindua meza kibabe wamekwama hivyo wanarejea kujipanga kwa ajili ya wakati mwingine.

“Tulipambana kwa ajili ya kutafuta matokeo na mipango yetu ilikuwa ni kupindua meza bahati haikuwa yetu kwa sasa tunarejea Bongo kuendelea kujipanga kwa ajili ya michezo ya Ligi Kuu Bara,” amesema Maganga.


1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic