December 28, 2019



MEDDIE Kagere mshambuliaji wa Simba guu lake limeibuka uwanja wa Uhuru baada ya kupita dakika 229 alizocheza bila kuzifumania nyavu kwenye mechi mbili alizocheza akiwa na Simba msimu huu.

Kagere amefunga mabao tisa mpaka sasa ni mabao matano amefunga kwa guu la kulia huku mawili akifunga kwa guu la kushoto na mawili kwa kichwa mara ya mwisho kufunga ilikuwa mbele ya Mbeya City wakati Simba ikishinda mabao 4-0 akifunga kwa guu la kulia kwa penalti iliyosababishwa na Miraj Athuman ‘Sheva’.

Alicheza dakika 229 bila kufunga bao mbele ya Tanzania Prisons mchezo ulokamilika kwa sare ya bila kufungana pia kwenye ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Ruvu Shooting hakufunga mpaka alipoifunga Lipuli dakika ya 49 na kufanya zitimie dakika 229 bila kufunga kwenye ushindi wa mabao 4-0 uwanja wa Uhuru.

Timu nyingine ambazo Kagere amezifunga ni pamoja na  JKT Tanzania wakati Simba ikishinda mchezo wake wa kwanza mabao 3-1 alipachika mawili kwa guu lake la kulia akimalizia pasi za mwisho za Mzamiru Yassin, mbele ya Mtibwa Sugar alipachika bao moja kwenye ushindi wa 2-1 kwa pasi ya Sharaf Shiboub.

Mawili alifunga mbele ya Kagera Sugar ambapo bao moja alifunga kwa kichwa akimalizia pasi ya Shomari Kapombe na moja kwa penalti iliyosababishwa na Miraj kwa guu lake la kulia.Lingine la kichwa alifunga mbele ya Azam FC uwanja wa Taifa kwenye ushindi wa bao moja akimalizia pasi ya Francis Kahata.

Pia aliifunga Biashara United kwa guu lake la kushoto akimalizia pasi ya Miraj wakati Simba ikishinda mabao 2-0 uwanja wa Karume na bao lake la nane ilikuwa kwenye ushindi wa mabao 4-0 mbele ya Mbeya City na bao lake la tisa alifunga kwa guu la kulia kwenye ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Lipuli.

Kagere ameliambia Championi Jumamosi kuwa kila siku anajipa changamoto mwenyewe ili kuwa bora.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic