ARSTICA
Cioaba, Kocha Mkuu wa Azam FC, leo anangia kikaangoni tena baada ya kupoteza
mechi yake ya pili akiwa kwenye benchi la ufundi ndani ya Azam FC kwa kufungwa bao 1-0 na Coastal Union ya Tanga.
Leo atakutana na timu ya Polisi Tanzania iliyotoka kushinda mabao 2-1 mbele ya KMC uwanja wa Ushirika, Moshi.
Mechi ya
kwanza kwa Cioaba ilikuwa dhidi ya Ruvu Shooting ambayo alikuwa ugenini na
alifungwa bao 1-0 mchezo wake wa pili kupoteza ilikuwa mbele ya Coastal
Union alifungwa pia bao 1-0 uwanja wa Mkwakwani.
Kocha Msaidizi wa Azam FC, Idd Cheche amesema kuwa
umakini ulikosekana katika kumalizia nafasi za mwisho.
“Ushindani
kwenye ligi ni mkubwa na kila timu inapambana kupata matokeo ila nina amini
tutafanya vizuri kwenye mechi zetu zinazofuata,” amesema Cheche.
Kocha mlimfukuza leo tena mmemrejesha wachezaji magarasa wameachwa na wenzenu mmeenda kuwaokota nyinyi
ReplyDelete