IMEBAINIKA
kuwa uongozi wa Polisi Tanzaia umepania kubana matumizi ya usajili kwa kusajili
wachezaji ambao wapo huru ili kupunguza gharama za uhamisho kwa mchezaji.
Polisi Tanzania ipo chini ya Kocha Mkuu wa Malale Hamsini ambaye amepewa kandarasi hiyo akichukua mikoba ya Seleman Matola ambaye amejiunga na Simba kwa sasa.
Habari
zinaeleza kuwa miongoni mwa malengo ya Polisi Tanzania ni kufanya usajili mzuri
ila usiwe wa gharama jambo lililowafanya waache nyota wengi waliokuwa kwenye
hesabu zao msimu huu.
“Kuna
wachezaji wengi wazuri ambao wanahitajika na Polisi Tanzania ila kwa sasa
hawatasajiliwa kutokana na kukwepa gharama ndio maana wanasajiliwa wale walio
huru kama ilivyo kwa Pius Buswita,” alieleza mtoa taarifa.
Ofisa Habari
wa Polisi Tanzania, Frank Lukwaro amesema kuwa wamejipanga kufanya usajili
makini ambao wataumudu kwa kuongeza jumla ya wachezaji wanne ambao wanahitajika
ndani ya kikosi.
“Tunahitaji
kusajili wachezaji wanne ambao tutawamudu na wenye uwezo wa kutosha, kwa sasa
tumemalizana na Buswita wengine wanakuja, tumebakiza wachezaji watatu tu kwenye
dirisha hili dogo,” amesema Lukwaro.
0 COMMENTS:
Post a Comment