January 17, 2020



BEKI wa Manchester United, Ashley Young imeripotiwa kuwa amegomea mazoezi ya timu yake akishinikiza kutimkia ndani ya kikosi cha Inter Milan.
Young amekubali kujiunga na Inter Milan inayoshiriki Serie A akitokea kwenye timu inayoshiriki Ligi Kuu England na anatarajia kufanyiwa vipimo hivi karibuni kukamilisha dili hilo.
Imeripotiwa kwamba nyota huyo hafurahishwi na maisha yake ndani ya Manchester United na mabosi wa Inter Milan wameweka mezani pauni milioni 15 kuipata saini yake.
Nyota huyo amegomea dili la kuongeza mkataba wa mwaka mmoja ndani ya United na anahitaji kuondoka kwenye usajili wa mwezi Januari licha ya mkataba wake kumeguka mwishoni mwa msimu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic