January 17, 2020


BERNARD Marrison, nyota mpya wa Yanga amesema kuwa amekuja Bongo kufanya kazi ndani ya Yanga wenyewe watampenda.

Marrison raia wa Ghana ambaye ni mshambuliaji, ametua leo nchini Tanzania akitokea nchini Ghana kwa ajili ya kumalizia taratibu za awali kuitumikia timu ya Yanga.

“Nimekuja rasmi ndani ya Yanga kufanya kazi na nina amini tutakuwa vizuri kutokana na ubora wa kikosi pamoja na sapoti ambayo tutaipata kutoka kwa mashabiki.

“Kikubwa ni sapoti kwani hakuna jambo jingine ambalo nimekuja kufanya zaidi ya kazi tu kwa sasa,” amesema.

Miongoni mwa timu ambazo amezipitia nyota huyo ni pamoja na DC Motemma Pembe, Orlando Pirates na  AS Vita.

4 COMMENTS:

  1. Leteni wapya kwa wingi muchukue ubingwa haraka

    ReplyDelete
  2. haya ni maneno ya waandishi na sio wachezaji, kila mchezaji akija wwaandishi wanashindwa hadi kubadilisha maneno. wanasahau kama walivyokuwa wanasahau darasani.
    hawa wanadanganya mashabiki na kujikuta wanachoona ni tofauti.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic