January 11, 2020


AISHI Manula, mlinda mlango wa Simba kwa sasa amekuwa gumzo kwa mashabiki kutokana na kile wanachoeleza kwamba amefungwa mabao mengi ya kizembe kwa mashuti makali na nje ya 18 kwa msimu huu wa 2019/20.

Kuna mengi ambayo yapo kwenye timu ila linapokuja suala la matokeo mazuri hakuna ambaye anamkubuka Manula ni mpaka pale atakapoboronga ndipo wengi wanamgeukia na kumtazama kwa jicho la pili.

Kabla sijafika mbali ndugu msomaji nikutakie kheri ya mwaka mpya 2020 kwa kuwa mambo yanazidi kusonga mbele taratibu ni muda wa kujipanga na kuona kwamba kila mtu anajua namna bora ya kutimiza malengo yake kwa wakati huu.

Kuna mengi ambayo umeyapanga kwa mwaka 2020 ni vema ukamtanguliza Mungu na kufanya mambo hayo kwa wakati ambao umejiwekea ili kutimiza ndoto zako ambazo unazifikiria kwa muda wote wa masiha yako.

Mashabiki wa soka wanapenda kuona matokeo chanya na yanapatikana ndani ya uwanja na sio nje ya uwanja vita ya manenomaneno muda wake umekwishwa kwa sasa ni wakati mwingine wa kuanza kufanya mambo bora kwa ajili ya kufikia mafanikio.

Turudi kwenye mada ya leo ambapo nipo na mlinda mlango wa Simba, Manula ambaye mashabiki wanamuona amechuja hana uwezo tena wa kukaa kwenye lango na badala yake nafasi hiyo apewa Beno Kakolanya.

Ni ngumu kumhukumu mlinda mlango huyo ambaye ni mlinda mlango namba moja ndani ya kikosi cha Simba anapambana na rafikiye Beno Kakolanya alijiunga na Simba msimu wa 2017 akitokea klabu ya Azam FC.

Kwenye mechi alizokaa langoni ambazo zimeikutanisha Simba na Yanga ni mechi sita mpaka sasa ambazo ni sawa na dakika 540 na hakufungwa na Yanga zaidi ya kulazimisha sare ama kushinda.

Kwenye jumla ya mechi hizo sita Manula hajapoteza mchezo hata mmoja zaidi ya kupata sare kwenye jumla ya mechi nne na kushinda mechi mbili.

Jumla ya mabao ambayo ametunguliwa Manula ni mabao matatu pekee na mechi ya Jumamosi inavunja rekodi kwa kufungwa mabao mengi ambayo ni mawili kwenye mechi moja alizokutana na Yanga.

Matokeo ya mechi ambazo Manula alikaa langoni zilikuwa namna hii:- 23/08/2017 hii ilikuwa ni ngao ya jamii, Simba 0-0 Yanga, 28/10/2017 hii ilikuwa ni ya ligi, Yanga 1-1 

Simba, 29/04/2018 ilikuwa ni ligi, Simba 1-0 Yanga, 
30/09/2018 ilikuwa ya ligi, Simba 0-0 Yanga, 16/02/2019 ilikuwa ni ya ligi, Simba 1-0 Yanga na Jumamosi, Januari 4,2020 mechi yake ya sita na ilikuwa ya ligi Simba 2-2 Yanga.

Hapa inaonyesha ni namna gani Manula amekuwa na uzoefu na mechi za Simba na Yanga kwa muda ambao amekaa ndani ya Simba mpaka sasa.

Kwa msimu huu Manula akiwa ndani ya Simba amekuwa chaguo la kwanza la makocha wote wawili alianza akiwa chini ya Patrick Aussems ambaye alikaa langoni kwenye mechi zote 10 sawa na dakika 900 na alifungwa mabao matatu pekee.

Katika mabao hayo matatu ni bao moja pekee alifungwa nje ya 18 ilikuwa mbele ya JKT Tanzania, bao hilo lilifungwa na Edward Songo wakati Simba ikiibuka na ushindi wa mabao 3-1 na mengine mawili yote alifungwa ndani ya 18.

Ikumbukwe kuwa wakati Manula anacheza na Ruvu Shooting aliweza kuokoa aina ya mashuti ya mbali na kuifanya ngome yake kuwa salama wakati wakiibuka na ushindi wa mabao 3-0 uwanja wa Uhuru.

Kwa bao lake la pili la mbali alilofungwa msimu huu bado si wakati wa kumpigia kelele na kuona kwamba hafai bado mpira ni mchezo wa makosa labda ndugu msomaji lile shuti la Mapinduzi Balama ungekuwa wewe ndiye Manula ungefanyaje?

Tumpe sapoti mtanzania mwenzetu na tujivunie vya kwetu, bado Tanzania ina walinda mlango wachache kama ilivyo kwa washambuliaji, ila Manula ndugu yangu nawe unapaswa ujifunze kupitia makosa.


2 COMMENTS:

  1. Huu ni ujinga hauna hata mantiki ya kujadili.Hakuns kipa asiyefungwa.Waandishi uchwara wameanzisha glo tonic ili mradi wapate cha kujadili.Anafuungwa DeGea magoli ya mbali na hakuna anayeshangaa kwani ni sehemu ya mchezo.Akiokoa mashuti mbona hamna makala za kumsifia???

    ReplyDelete
    Replies
    1. Sahihi kabisa,kwa nini hawamsifii kwa kuandaa makala anavyofanya vizuri?..

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic