January 30, 2020


KOCHA Mkuu wa Mtibwa Sugar, Zuber Katwila amesema kuwa timu ya Sahare Stars ipo vizuri na ikipambana itafikia malengo iliyojiwekea.
Sahare iliwanyoosha Mtibwa Sugar kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya 32 bora kwa kuwaondoa kwenye reli vigogo hao wanaoshiriki Ligi Kuu Bara kwa ushindi wa penalti 3-2 baada ya kutoshana nguvu ya kufungana bao 1-1 ndani ya dakika 90.
 Katwila amesema kuwa walicheza vizuri na walionyesha ushindani jambo lililowapa nafasi ya kusonga mbele.
"Tulikuwa na changamoto kutoka kwao na ushindani ulikuwa mkubwa. Tumetolewa kwa penalti tumekubali kushindwa kwani tulikuwa nyumbani na mpira umechezwa wanastahili pongezi nasi tunajipanga kwa ajili ya mechi zetu nyingine zinazofuata," alisema.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic