January 10, 2020



BEKI ya NMB imewapiga tafu wana michezo wa Visiwani Zanzibar kwa kutoa vifaa vya michezo kwa ajili ya kusherehekea  miaka 56 ya Mapinduzi.


Zoezi hilo la kukabidhi vifaa hivyo limefanywa na Meneja wa NMB tawi la Zanzibar, Abdallah Duchi ambaye alimkabidhi vifaa vya michezo Salim Ali Jazira kwa ajili ya timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

Vifaa hivyo ni pamoja na Jezi na Mipira kwa ajili ya michezo ya kusherehekea miaka 56 ya mapinduzi ya Zanzibar.

 Thamani ya vifaa hivyo ambavyo ni kwa ajili ya Mpira wa Miguu na Kikapu vyote ni shilingi milioni 6.5. Hafla ya makabidhiano ilifanyika kwenye ukumbi mdogo wa Baraza la Wawakilishi Chukwani Zanzibar jana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic