January 3, 2020






Kampuni ya Star Media kupitia brand yake ya StarTimes, imepata kibali cha kuonyesha michuano ya Kombe la FA (Emirates FA Cup) ikianza na ufunguzi wake kwa maana ya mchezo wa Ngao ya Jamii (FA Community Shield) ambapo watakuwa wakirusha matangazo ya mechi zote mubashara kutoka nchini Uingereza.


Akitoa ufafanuzi wa kibali hicho Meneja Masoko wa kampuni hiyo, David Malisa amesema,StarTimes imepata rasmi kibali hicho ambacho itakuwa ni mahususi kwa kurusha michezo hiyo katika nchi zote za Kusini mwa  Jangwa la Sahara kupitia lugha mbalimbali kibali ambacho kitadumu mpaka mwishoni mwa mwaka 2021.


“Kwa niaba ya Mkurugezi wetu wa Idara ya Michezo kutoka makao makuu yaliyopo Beijing China, Shi Maochu ametuambia kuwa, hii ni hatua kubwa kwa michuano ya Emirates FA na Emirates Community Shield kurushwa kwetu, kwa sababu yanajumuisha timu zote kubwa na bora  zilizopo nchini Uingereza, hivyo tunafuraha kubwa sana kuwa sehemu ya kuonyesha michuano hiyo.




“Tunatambua wazi kuwa Watanzania wengi ni wapenzi wa mpira wa miguu, hivyo kwa kutambua hilo na ndiyo maana nasi tumezingatia hili kwa kuwasogezea matangazo yetu karibu  ambapo watapata burudani ikiwa ni sambamba na michuano   ya kimataifa ya Copa Italia, na Bundesliga lakini pia  baadhi ya ligi za Ulaya kama UEFA Europa League na Euro 2020.


Malisa aliongeza kwa kusema kuwa: “Pamoja na uwepo wa michuano mingi na mikubwa kama hiyo, tutaendelea kuwaletea maudhui mbalimbali kwa gharama nafuu kabisa hususani ndani ya mwaka huu wa 2020 ili tuweze kukidhi matarajio ya watazamaji wetu kwani mashindano haya ya Kombe la Emirates FA 2019/2020 yataanza kurushwa rasmi  Januari 4 mwaka huu kwa maana ya kesho Jumamosi kupitia king’amuzi pendwa cha StarTimes.


“Lakini lazima watazamaji wetu wakumbuke kwamba matangazo haya yatakuwa mubashara kupitia chaneli 8 za michezo zilizopo kwenye king’amuzi chetu ila pia tutarusha kupitia APP yetu ya StarTimes on live, hivyo unatakiwa kulipia mapema king’amuzi chako  kupitia bando la Uhuru kwa shilingi 18000 tu hili kwa watumiaji wa Antenna na shilingi 21000 kwa watumiaji wa Dish,” amesema Malisa.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic