January 12, 2020



BAKARI Shime, Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania ya Wanawake chini ya miaka U 17 amekiongoza kikosi chake kupata ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Burundi kwenye mchezo wa kuwania kufuzu tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia kwa Wanawake.

Mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar, leo, Januari 12, ulishuhudiwa na mashabiki wengi waliojitokeza kuipa sapoti timu hiyo ambayo imecheza soka la pasi nyingi na kushambulia.

Asha Masaka mshambuliaji wa U 17 alikuwa mwiba kwa safu ya ulinzi ya Burundi na mlinda mlango wao, Amissa Inarukundo ambaye aliokoteshwa nyavuni mabao matatu ya Asha aliyesepa na mpira wake huku Joyce Meshack na Protasia Mbunda wakipachika bao mojamoja na kukamilisha jumla ya mabao matano kwa U 17 ya Tanzania.

Bao pekee la kufuta machozi kwa Burundi lilipachikwa na Nadine Ndayishimiye kutokana na uzembe wa safu ya ulinzi wa timu ya Taifa ya Tanzania, U 17.

 Michuano hiyo inatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu nchini India na mchezo wa marudio unatarajiwa kufanyika Januari 25, nchini Burundi.

Shime amesema kuwa sapoti kubwa ya watanzania imechangia kupata ushindi na vijana wamepambana kupata matokeo na malengo ni kushiriki kombe la dunia kwa kuanza kuyafanyia kazi makosa waliyoyafanya Uwanja wa Taifa. 

Peace Olga nahodha wa Burundi amesema kuwa kilichowaponza ni ukubwa wa uwanja pamoja na nyasi bandia walizozizoea kwao tofauti na Taifa

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic