February 22, 2020



HITIMANA Thiery, Kocha Mkuu wa Namungo FC amesema kuwa sare ya kufungana bao 1-1 ya Azam FC mbele ya Ndanda FC inampa hofu ya kujipanga kukabiliana na wapinzani wake.

Namungo FC itamenyana na Azam FC leo, Uwanja wa Majaliwa ikiwa na kumbukukumbu ya kushinda mabao 2-1 mbele ya KMC.

Akizungumza na Saleh Jembe, Thiery amesema kuwa ni ngumu kwa timu yenye uzoefu kama Azam FC kulazimisha sare kwenye uwanja mgumu wa Nangwanda jambo ambalo linamfanya atafute mbinu za kuizuia.

“Niliutazama mchezo wa Azam, mwanzo mwisho walikuwa wanasukuma mashambulizi na kucheza kwa mbinu tofautitofauti, kwa namna wanavyocheza na uzoefu walionao nitatumia nguvu nyingi kuwazuia jambo ambalo litaongeza ugumu wa mchezo.

“Kikubwa ambacho ninakifanya kwa sasa ni kuwaandaa wachezaji wangu kisaikolojia watambue kwamba wanakutana na timu imara na yenye kasi muda wote wasikumbuke ushindi wao uliopita,” amesema.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic