LEO Uwanja
wa Taifa, Simba itawakaribisha Biashara United kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara
utakaochezwa majira ya saa 1:00 usiku.
Balaa kubwa
lipo kwenye idadi ya mabao ya kufunga kwa timu ya Biashara United iliyo chini
ya Francis Baraza imefunga mabao 15 kwenye mechi 22 ilizocheza huku Simba
ikifunga mabao 47 kwenye mechi 23 ilizocheza.
Achana na
mabao hayo, ukichukua mabao ya Meddie Kagere mwenye mabao 13 na mabao ya Jonas
Mkude mwenye mabao mawili unapata idadi ya mabao 15 ya Biashara United.
Simba
inayonolewa na Sven Vandenbroeck ipo nafasi ya kwanza na pointi 59 na Bishara
United ipo nafasi ya tisa ina pointi 32.







0 COMMENTS:
Post a Comment