March 4, 2020


ADOLF Riashard, Kocha Mkuu wa Tanzania Prisons amesema kuwa wachezaji wapo tayari kunaliza biashara leo mbele ya Biashara United.
Prisons iliyo nafasi ya 11 ikiwa na pointi 34 baada ya kucheza mechi 25 itamenyana na Biashara United iliyo nafasi ya 9 ina pointi 35.
Akizungumza na Saleh Jembe, Rishard amesema kuwa vijana wake wapo tayari kupambana na Biashara United anaamini watafanya vizuri.
“Ushindani ni mkubwa na kila timu inaingia uwanjani ikihitaji pointi tatu lakini sisi tupo tayari kuzipata kwa kucheza soka safi, mashabiki wajitokeze kwa wingi kutupa sapoti,” amesema.
Prisons inaongoza kwa timu zenye sare nyingi ndani ya Ligi Kuu Bara ikiwa nazo 13 ambazo ni sawa na dakika  1,170

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic