OFISA Mtendaji Mkuu wa
Azam FC, Abdulkarim Amin 'Popat' amesema kuwa wamewaacha nyota wao watatu ndani ya kikosi hicho ikiwa ni mpango wa kufanya maboresho ndani ya kikosi hicho.
Jana, Julai 30, Azam FC ilimtambulisha kiungo Awesu Awesu kwa dili la miaka miwili akiwa ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na Kagera Sugar.
"Yote tunayofanya ni mapendekezo ya kocha Arstica Cioaba ambaye anahitaji kuwa na kikosi bora msimu ujao, bado tunaendelea kuboresha kikosi kwa mapendekezo ya benchi la ufundi," amesema.
Awesu alikuwa kwenye rada za Yanga ambao wameikosa saini ya nyota huyo mwenye mabao saba kwenye mashindano yote ndani ya msimu wa 2019/20.
Aliwahi pia kukipiga ndani ya Azam FC wakati alipokuwa kwenye Academy ya Azam FC 2014/15 kabla ya kuondoka na kuibukia Arusha.
0 COMMENTS:
Post a Comment