AZAM FC inayonolewa na Arstica Cioaba raia wa Romania, leo Agosti 27 inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya KMC.
Mchezo huo utapigwa majira ya saa 1:00 usiku Uwanja wa Azam Complex.
Lengo la mchezo huo ni kujiweka sawa kwa ajili ya ligi kuu inayotarajiwa kuanza Septemba 6 na Azam FC wao watafungua pazia na Klabu ya Polisi Tanzania.KMC jana ilicheza mchezo wa kirafiki na Klabu ya Simba, Uwanja wa Uhuru na ilipoteza kwa kufungwa mabao 3-1 hivyo leo utakuwa ni mchezo wake wa pili nao pia wakijiweka fiti kabla ya ligi kuanza.
0 COMMENTS:
Post a Comment