August 15, 2020

 
LARRY Bwalya kiungo aliyekuwa anakipiga ndani ya Power Dynamo ya Zambia amemalizana na Simba kwa dili la miaka miwili leo Agosti 15.

Nyota huyo ametua leo Bongo kwa ndege ya shirika la Ethiopia Airlines na kumalizana na Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania.


Nyota huyo ana uwezo wa kutumia mguu wa kushoto anaungana na kiungo mwenzake mnyumbulifu Clatous Chama, mwamba wa Lusaka ambaye naye anatokea pia Zambia.


Chama amekuwa na msimu mzuri kwa mwaka 2019/20 akitwaa tuzo ya mchezaji bora na kiungo bora anaungana na kiungo huyo ambaye anapewa nafasi kubwa ya kuongeza nguvu kwenye kikosi hicho kitakachoiwakilisha nchi kwenye michuano ya kimataifa.

18 COMMENTS:

  1. Mbona kinyonge hivyo Saleh Jembe ulitegemea nini?Kama huna pesa unakuja na bla bla ndio matatizo yake.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Barua ya wazi kwenda klabu ya simba.Mimi nnahisi kwa kiasi kikubwa watanzania tunakosa kujiamini kwenye maeneo yetu ya kiutawala ninaamanisha kwenye nafasi yetu ya kuweka alama ya maendeleo katika Dunia hii kama wanafamilia wa Dunia hii.Na ndio maana tunamsumbua Maguful kwa maneno ya kejeli wakati wenzetu wa nchi za nje wanamuundia maktaba ya kitafiti kumsoma kujua chanzo cha uwezo na ujasiri alionao. Juzi moja nilimsikia Khaji Manara akisema anataka ikifika 2050 watanzania karibu wote wawe wapenzi wa Simba? Yaani miaka 30 kutoka sasa.Lakini ukija kwenye hesabu za kiutendaji za Magufuli Simba wanaweza kufikia azma hiyo ndani ya miaka mitano au kumi. Mimi nilijiuliza sana kwanini watanzania na watu wa mataifa mengine wanazisapoti timu za mataifa ya ulaya? Bila shaka kuna kitu walifanya watu wa ulaya kuwavutia watu wa mataifa mengine kushabikia timu za ulaya. Lakini bila ya utafiti wa kina unaweza kusema timu za mataifa ya ulaya yamepata mashsbiki wengi wa nje ya ulaya kutokana na kuwahi teknojia ya TV.Mechi nyingi za timu za ulaya kupitia ligi zao ziliweza kuonekana laivu kupitia tv Duniani kote.Jambo la pili ni kwamba timu za ulaya ni miongoni mwa vilabu nya mwanzo kuajiri wachezaji wa mataifa ya kigeni na kuweza kuvuna sapota za watu wa asili ya wachezaji hao wa kigeni walipotoka. Na hapa ndipo kuna jambo letu la kuelezea kitu kidogo.Kama ligi yetu ya Tanzania inaonekana laivu karibu nchi nyingi za ukanda wa Africa mashariki na kati, na timu kama ya simba yenye wachezaji wa kigeni wa karibu kila taifa linaloizunguka Tanzania kwanini wasieke malengo ya kuvuna wanachama na mashabiki wa maeneo hayo? Kuna rasilimali kubwa ya watu kwenye hayo maeneo ya kufanya bishara ya jazi na vitu vyengine hakuna kisichowezekana. Cha kufanya Simba ni kufanya vyema kwenye klabu bingwa Africa kwani ukanda wetu huu wa Africa mashariki na kati hadi kusini una njaa ya timu kufanya vyema kwenye mashindano hayo makubwa Africa kwa ngazi za vilabu. Simba wana Lou miqisoni hapo tunazungumzia msumbiji. Wana chama na bwalya.tunazungumziazambia.wana kahata na Onyango hapo tunazungumzia Kenya.pengine simba pia wakawa na wakongo. Bila ya kusahau kagere tunazungumzia Rwanda.kwa upande wa waganda Simba zamani tu ana mashabiki wengi kule.Nadhani hata huyo Senzo alikuwa anakula pesa zisizo stahiki kwani Africa mashariki kuna potential kubwa ya timu kama simba kujitanua na kunufaika kiuchumi. Simba wanatakiwa kuepuka falsa ya Mazembe ya kuridhika na nyumbani kwani licha ya mafanikio makubwa ya Tp Mazembe kwenye soka la Africa lakini timu hiyo imeshindwa kujitanua Africa kimashabiki licha ya timu hiyo kuundwa na wachezaji wengi kutoka kila pembe ya Afrika.
      20% per cent aliimba kwenye tamasha la CCM kuwa yale watanzania tuliokuwa tunaona kuwa hayawezekani kwa miaka mingi kumbe yanawezekana na yale yaliokuwa watanzania tunaona hayawezi kuonekana kwa miaka mingi kumbe yanaonekana na Magufuli ndie aliethibitisha hayo kwa vitendo tena kwa kipindi kifupi tu. Watanzania tuamke kwani kwenye ukanda huu wa Africa hakuna mtu jasiri kama Mtanzania na huo ndio ukweli. Na ndio maana kuna makaburi ya watanzania kwenye nchi kadhaa za kiafrika ya mashujaa wetu kuipigania Uhuru wa Africa.Kama watanzania tuliongoza vita ya kuikomboa Africa kisiasa tukashinda vita. Kwa kweli wakati umefika sasa kuacha uoga kudhamiria kujikomboa kimaendeleo ya kweli kunako kila nyanja na kuziongoza nchi nyengine za kiafrica kufuata nyayo zetu maana nchi halisi ya kiafrica kwenye ukanda huu ni Tanzania pekee nyengeine zote kama hazijatawaliwa kitamaduni na mataifa ya nje basi yametawaliwa Kilugha na kiuchumi.

      Delete
  2. walter Bwalya ataenda yanga kwa dola 25000 tu
    wanapenda dezo...kwa Tshishimbi wameshindwa kujiongeza

    ReplyDelete
  3. Nimekuwa nawauliza weredi wa huyu mwandishi Salehe Jembe ,aliweka two Bwalya mmoja yupo Egypt na mwingine Power Dynamo Mimi kwa akili yangu huyu ni Simba niliuliza na huwezi amini taarifa yangu haikutoka cse nilijua ana maanisha nini ? hapa Elimu tu

    ReplyDelete
  4. Kweli so Kiongozi lkn jpime maadili yenu ,Simba Kama Mwarabu na Mpemba mtu anazaa bila kuongeza idadi

    ReplyDelete
  5. Kauli mbiu ya Utopolo "Laumu vyote venye uhai bila sisi kuwajibika"
    Yaani wao kila siku ni kulaumu tu.Hwta tetemeko la ardhi la hivi karibuni ni kosa la jamwti ya sheria na hadhi ya wachezaji.
    Hata siku moja wao(Utopolo)hawakosei wala kuwajibika.

    ReplyDelete
  6. Nahofia grading ya Media hasa micheZo Simba inapamgwa Sana Amina

    ReplyDelete
  7. Wewe unayeita Yanga Utopplo umelala na mkeo unasingizia mafumanizi

    ReplyDelete
  8. Bwala mchezaji nzr ni sw kbs lkn mhm zaidi kwa sasa wanasimba wenzangu kwny timu yetu ni striker ht mmoja mkali bs mshamaliza usajili! By the way hatuna mshindani bongo lbd nje ya nchi!!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mpira wa kisasa unategemea zaidi viungo ambao wenzetu wanawaita false strikers. Kwa mfano Simba Ina viungo wengi wenye uwezo wa kufunga Kama chama, miquisone, kahata na Sasa Bwalya.

      Delete
  9. Bwala mchezaji nzr ni sw kbs lkn mhm zaidi kwa sasa wanasimba wenzangu kwny timu yetu ni striker ht mmoja mkali bs mshamaliza usajili! By the way hatuna mshindani bongo lbd nje ya nchi!!

    ReplyDelete
  10. Bwala mchezaji nzr ni sw kbs lkn mhm zaidi kwa sasa wanasimba wenzangu kwny timu yetu ni striker ht mmoja mkali bs mshamaliza usajili! By the way hatuna mshindani bongo lbd nje ya nchi!!

    ReplyDelete
  11. Saleh jembe huwa haitendei haki blog yake kutokana na mahaba aliyonayo dhidi ya yanga

    ReplyDelete
  12. Sasa Mimi naomba kwa kazi yangu ya kihuni nikwambie u a unprofessional Amina am

    ReplyDelete
  13. Unapenda Yanga ila jiongeze akkili yako

    ReplyDelete
  14. Shida ya Timu inaitwa Simba wapenzi wake siku zote wanyoa hooo hongera Kaka sarehe' lkn inakuwaje Yanga wakiibuka na Over Chama idea ?au utaendelea na toleo la tatu Molinga ,lkn ukweli nimeamini Wazungu walo tutawala hawakuwekeza kwenye michezo ndo maana makabila yote yenye zero Utawala yanazalisha Waandishi wa michezo

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic