September 23, 2020


 

TIMU ya Mwadui FC imekwama kufurukuta kwenye mechi zake tatu za mwanzo kwa msimu wa 2020/21 baada ya kuyeyusha pointi sita jumlajumla.


Mchezo wake wa kwanza kwa msimu huu ilianza kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 mbele ya Biashara United ilipokuwa ugenini Uwanja wa Karume.


Mchezo wake wa pili ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0 mbele ya Dododma Jiji FC Uwanja wa Jamhuri Morogoro na mchezo wake wa tatu ilipoteza kwa kufungwa na KMC FC mabao 2-1 ikiwa Uwanja wao wa nyumbani wa Mwadui Complex.

Ndani ya dakika 270 imeyeyusha pointi sita huku ikifunga bao moja na kufungwa mabao manne.

Matokeo yake yalikuwa namna:-Biashara United 1-0 Mwadui FC, Karume.

Dodoma Jiji 1-0 Mwadui, Jamhuri, Dodoma.

Mwadui 1-2 KMC, Mwadui Complex, Shinyanga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic