October 16, 2020


CEDRICK Kaze, Kocha Mkuu wa Yanga ambaye ametua Bongo usiku wa kuamkia leo amesema kuwa anachohitaji ndani ya Yanga ni sapoti ili aweze kufikia malengo ambayo Yanga wanahitaji.


Kaze amekuja kuchukua mikoba ya Zltako Krmpotic ambaye alifutwa kazi Oktoba 3 na uongozi wa Yanga.Na ameweka bayana kuwa amekuwa akipokea meseji nyingi kutoka kwa mashabiki.


Kaze amesema:"Ninaweza kusema kuwa nimepata faraja kubwa sana kuwa kocha wa Yanga na wengi wamekuwa wakinipongeza katika hili na meseji nimepokea nyingi sana.


"Kikubwa ambacho ninaweza kusema ni kwamba nimekuja kufanya kazi na ninachohitaji ni kuona wengine wanasapoti kazi yangu katika hili.


"Yanga ni timu kubwa na ina mashabiki wengi hivyo kinachotakiwa kwa sasa ni kuangalia namna gani tutafikia mafanikio na malengo ambayo tumejiwekea," amesema.

8 COMMENTS:

  1. Watafukuzwa Sanaa sababu yanga inawachezaj wazuri ila wenyewe wachezaji wanaprexha na badala yake wanashindwa kuturiza presha na kucheza mpira wapasi kama simba na kupata matokeo

    ReplyDelete
  2. Kwan simba inayocheza mpira wa pasi Ina point ngapi na yanga ambayo haichezi mpira wa pasi Ina point ina point ngapi? Kikubwa ni matokeo yanayokupa point

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kama kikubwa ni matokeo mbona wamefukuza kocha

      Delete
  3. Hawa jamaa ni ndugu au????

    ReplyDelete
  4. Atafukuzwa huyo tarehe 7 subirini mtaona

    ReplyDelete
  5. kelele hatutaki mctupangie akizingua tunafukuzaaa!!!

    ReplyDelete
  6. Yanga akifukuza na akiajiri kocha mwngne simba kuna hela wanachangia labda?

    ReplyDelete
  7. Simba Wana uchungu wa mimba inakataa kutoka,tufanye operation mama hawezi kusukuma mwenyewe

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic