November 9, 2020


 KOCHA Msaidizi wa Gwambina, Athuman Bilali ‘Bilo’ amesema timu yake haitatoa likizo kwa wachezaji wake kwakuwa malengo ya timu yake ni kurekebisha makosa yanayojitokeza kwenye timu hiyo ili waweze kupata matokeo kwenye michezo ya ligi kuu.


Kwa sasa Ligi Kuu Bara na Ligi Daraja la Kwanza imesimama kwa muda kwa ajili ya mechi za timu ya Taifa, timu ya Tanzania Taifa Stars itamenyana na Tunisia Novemba 13, nchini Tunisia. 

Bilali ambaye ni kocha wa zamani wa Stand United amesema “:Kama benchi la ufundi la Gwambina tumeamua kutotoa mapumziko yoyote kwa wachezaji wetu tumepanga mazoezi yetu kuendelea katika kipindi hiki cha mapumziko na sisi tutaendelea kupambana mpaka mwisho.

 

“Kwenye michezo miwili ambayo tumecheza kwenye uwanja wetu wa nyumbani mmoja tumefungwa bao 3-0 na KMC na mwingine tukapata sare ya bila kufungana na Yanga, kiufundi timu yetu bado tunafanya makosa mengi ambayo tunatakiwa kuyapunguza tukiwa mazoezini.

 

 “Hivyo naamini kwamba ligi ikirejea tutafanya vizuri zaidi kwakuwa makosa yatakuwa yamepungua.

 

“ Nawaomba wapenzi na mashabiki wa Gwambina waendelee kuisapoti timu yao kuhakikisha inafanya vizuri na sisi kama viongozi wa benchi la ufundi tutaendelea kupambana na kufanya mabadiliko makubwa,” amesema Bilal.

 

   

     

     


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic