TIMU ya
Taifa ya Tanzania, chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes leo imeibuka na ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya Djibouti kwenye mchezo wa Michuano ya Cecafa uliochezwa Uwanja wa Black Rhino Academy,
Arusha.
Abdorahman Kamil dakika
ya 14 wa Djibouti alianza kupachika bao la kwanza ambalo lilidumu mpaka mapumziko na kuwafanya Ngorongoro Heroes kwenda kutafuta mbinu mpya kupata ushindi.
Chini ya
Jamhuri Khwelo, ‘Julio’ ambaye ni Kocha Mkuu wa Ngorongoro Heroes, mambo
yalibadilika dakika saba mbele baada ya kipindi cha pili kuanza baada ya Teps
Theonasy kupachika bao la kwanza dakika ya 52.
Mabao mengine yalifungwa na Abdul Hamis ambaye alifunga 'hat trick' mabao yake alifunga dakika ya 63,72 na 90 kwa mkwaju wa
penalti.
Khelfin
Hamdoum naye alikuwa miongoni mwa watupiaji alifunga bao dakika ya 82 pamoja na
Andason Kimweli kwenye mchezo wa ufunguzi uliokuwa na ushindani mkubwa.
Michuano hii
ambayo Tanzania ni wenyeji inashirikisha timu tisa ambazo ni pamoja na Kenya,
Sudan, Uganda, Sudan Kusini, Somali, Djibouti, Ethiopia,Burundi na wenyeji
ambao ni Tanzania.
0 COMMENTS:
Post a Comment